Kununua hisa nikiwa nje ya Tanzania?

Watanzania wanaoishi nje ya nchi wana fursa ya kuwekeza kwenye masoko ya mitaji hapa nchini kwenye masoko ya awali na pia kwenye masoko ya pili. Wanaweza kushiriki kwa kumchagua dalali wake ambaye atakuwa anamsaidia kuwekeza. Mwekezaji anatakiwa kuwa na mkataba na dalali wa kumsaidia kuwekeza akiwa nje ya nchi. Mkataba huo utabainisha jinsi ya kupokea fedha na namna ya kuidhinisha manunuzi au uuzaji wa hisa